Yesu ni nani?

Watume wa Agano La kale wanatueleza kuhusu kuja kwa Massia

Isaya

Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, baba wa milele, Mfalme wa amani.  Isaya 9:6

Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli-maana yake Mungu pamoja nasi.  Isaya 7:14 na Mathayo 1:22-23

Danieli

Nikaona katika njozi za usiku na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye. Naye akapewa mamlaka, na utukufu na ufalme, ili watu wa kabila zote na taifa zote na lugha zote wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, amabayo hayatapita kamwe na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.  Danieli 7:13-14.

Katika Agano Jipya

Mwana wa Mungu

Akawaambia, “Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?” Simoni Petro akajibu akasema, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” Yesu akajibu, “akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hiliu, bali Baba yangu aliye mbinguni.”  Mathayo 16:15-17.

Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu,bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu.  Yohana 5:17-18

Yesu akajibu; “Mimi na Baba tu umoja.” Basi Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige, lakini Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe? Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda,” bali ni kuwa umekufuru. “Wewe ingawa ni mwanadamu unajufanya kuwa Mungu.’’  Yohana 10:30-33

Baada ya kukamatwa na kutiwa nguvuni, viongozi wa Wayahudi wakauliza; “Wewe basi ndiye Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mmesema kwamba Mimi ndiye.’’  Luka 22:70

Aliyefufuka

Ingawa milango zilikuwa zimefunguwa, Yesu alikuja na kusimama katikati yao na kusema, “Amani iwe nanyi’’. Kisha akamwambia Thomasi “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyosha mkono wako uguse ubavuni Mwangu. Usiwe na shaka bali uamini tu.” Thomasi akamwambia, “Bwana wangu na Mungu Wangu!” Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.’’ Yohana 20:26-29

Nikamwona mtu kama, “Mwana wa Adamu’’ amevaa joho refu na mkanda wa dhahabu umefungwa kifuani mwake. Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto. Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama vile imesafishwa katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama sauti ya amji mengi. Katika mkono wake wa kuume alishikilia nyota saba na kinywani mwake ulitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake kama jua kali linalong’aa kwa nguvu zake zote.

Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akaweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema, “Usiogope, Mimi ni wa Kwanza na wa Mwisho. Mimi ni yeye aliye hai, niliyekuwa mimekufa na tazama ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.” Ufunuo wa Yohana 1:13-18

Unaweza pata uhai kwa Jina lake

Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele ya wanafunzi wengi Wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki. Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu na kwa kumwamini mpate uzima katika Jina Lake.  Yohana 20:30-31




Moyo wa ujumbe wa Biblia

Hadithi ambozo zifuatozo kukamata moyo wa ujumbe wa Biblia kwa njia mpya.

1. Dereva

Dereva mmoja alisimamishwa na afisa wa polisi. Alikuwa dereva stadi na kwa mujibu wa ufahamu wake hakuwa amekiuka sheria za trafiki.

Afisa wa polisi akasema, “nilikuweka kando kwa sababu ulikuwa ukiendesha gari kwa kiasi ya kilomita 55 kwa saa katika eneo la shule. Palikuwa na tangazo ya sheria kumi za kutahadharisha kuwa kiasi ya juu inayokubaliwa ni kilomita 15 kwa saa lakini ulizipuuza zote.”

Kwa vile dereva huyo alivyokuwa na ishara kumi za kumuonya, Mungu ametupa ishara kumi zilizo wazi za tahathari katika Bibilia. Zinajulikana kama Amri Kumi.

Je, umewahi kusema uongo, kuiba kitu au kutumia jina la Mungu kwa mzaha? Ikiwa u kama mimi, jawabu ni ndio.

Sikiliza Bibilia inavyosema:
Yeyote awekaye sheria yote lakini anajikwaa kwa moja amevunja yote
.   Jakobo 2:10

Mungu anasema kuwa kuivunja amri moja tumefanya dhambi na tutatakiwa kutoa hesabu kwa kuvunja amri zote, hata ile ya usinzi na uuwaji.

Hukumu ya Mungu kwa dhambi zetu ni kifo. (kutupwa jehanamu kwa sababu hatakubalia dhambi mbele ya uwepo wake).   
Warumi 6:23a

Kama hadithi hii ikiishia hapa, hakuna tumaini kwetu…


2. Mhukumiwa

Mtu aliyekuwa na hatia alimuendea hakimu na kujitolea kuuawa kwa niaba ya muuaji aliyapatikana na hatia. Hakimu alikubali.

Siku iliyofuata hakimu alimuambia mhukumiwa kuwa alikuwa na uamuzi wa kufanya.

“Mtu asiye na hatia ameuawa badala yako. Ikiwa utakubali fidia yake kwa kosa lako, una uhuru wa kuenda.

Ikiwa hutakubali fidia yake, utauawa kwa kosa lako. Umechagua lipi?”

Yesu Kristo, Mwana wa Mungu ingawa hakuwa na dhambi, aliutoa uhai wake kwa hiari ili kulipia adhabu zako na zangu. (Hukumu ya Mungu kwa dhambi zetu ni mauti). Siku tatu baadaye alifufuka kutoka kwa wafu.

Mungu alidhihirisha upendo wake mkuu kwetu kwa kumtuma Yesu ili afe kwa ajili yetu tulipokuwa tungali wenye dhambi.   Warumi 5:8

Kipawa cha Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.   Warumi 6:23b

Kutokana na kifo cha Yesu kwa niaba yako, una maamuzi mawili:

Pokea msamaha wa Mungu kwa dhambi zako pamoja na uzima wa milele kwa kutubu (kutambua hali yako ya dhambi na kutamani kutoka katika hali hiyo) na kuweka tumaini lako katika Bwana Yesu. (Matendo ya Mitume 20:21)

Au

Kukataa msamaha wa Mungu kwa dhambi zako pamoja na uzima wa milele kwa kumtumaini yeyote au chochote ila Yesu ili akufanye au kikufanye ukubalike kwa Mungu. Hivyo basi wewe mwenyewe ubebe adhabu kwa kuvunja sheria.

Kwa vyovyote vile wanaoamini katika mwana wana uzima wa milele, lakini yeyote anayemkataa Mwana wa Mungu hatauona uzima, kwa kuwa ghadhabu ya Mungu imekaa juu yake.   Yohana 3:36

Kujua kuhusu Yesu hakumaanishi unamuamini...


3. Mruka Angani

Waruka angani hudhihirisha imani yao katika miamvuli wanapovuka kutoka kwa ndege.

Wafuasi wa Yesu hudhihirisha imani yao kwake Roho wa Mungu anapowabadilisha katika mawazo na shauku zao.

Yeyote aliye katika Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yameisha, na yamekuwa mapya!   2 Wakorintho 5:7

Mungu asema, “
Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu.”   Ezekieli 36:26

Kama vile kuingia katika kiwanda hakuwezi kukufanya kuwa fundi wa magari, kuhudhuria kanisani hakutakufanya Mkristo.

Ikiwa ungependa kuupokea msamaha wa Mungu kwa dhambi zako na kipawa cha uzima wa milele, tafakari kuhusu kufanya ombi lifuatalo:

“Yesu, naamini ulilipa adhabu ya dhambi zangu ulipokufa msalabani na kufufuka kutoka kwa wafu. Nataka kugeuka kutoka kwa dhambi zangu na kuweka tumaini langu kwa Bwana wangu. Nataka kukufuata katika maisha yangu yaliyobaki. Amina.”

Yeyote anayeliitia jina la Bwana ataokoka.   Warumi 10:13

Wafuasi halisi wa Yesu huwa na shauku ya:

Kuishi maisha yanayolingana na uungu, kupendeza Mungu kwa njia zote, kuzaa matunda katika kazi zote vyema na kukua katika kumjua Mungu. Wakolosai 1:10

http://www.tracts.com/Kiswahili.html